Pengo la kufanikiwa kati ya wanafunzi wa kipato cha chini na mabaki ya kikundi cha wanafunzi huko Maine ni pana, inaendelea, ni mbaya, na ninge penda kuuliza msaada wa jamii katika kushughulikia shida hii muhimu.
Wataalamu wa shule wanajitahidi kuwasaidia wanafunzi wote kufikia viwango vya juu zaidi, lakini hawawezi kufunga pengo la kufanikiwa peke yao – tunahitaji wazazi kutusaidia. Kwa wakati huu wa mwaka, wakati wengi wetu tunatoa maazimio ya Mwaka Mpya, ningependa kupendekeza kuwa uingiliaji wa Mwaka Mpya wa jamii, uwe na kusudi la kushinikiza wanafunzi wote wafikie kutimiza kielimu kwa kiwango cha juu.
Ushahidi unaonyesha kwamba kusoma kwa ukawaida kwa upande wa wanafunzi ni muhimu kwa kufaulu kielimu, lakini walimu wanaona kuwa watoto wengi hawasomi kwa kila mara nyumbani. Kwa sababu kusoma kuna uhusiano wa karibu sana na kufanikiwa, wacha basi tufanye azimio linalo zingatia kusoma – Kwamba tutahakikisha watoto wetu, kwa umuri wowote ule walio nao, wanasoma nyumbani angalau kwa dakika 30 kila siku.
Wazazi wana ratiba zenye shughuli nyingi, najua. Wengi hufanya kazi mbili na tatu na bado wanajipiganisha kupata mapato. Bado hakuna kitu cha muhimu kama maisha ya baadaye ya watoto wetu. Na mpaka watoto watengeneze tabia ya kusoma, wanahitaji watu wazima kuhakikisha wanasoma kila wakati. Kwa hivyo, acha tufanye azimio la jamii kwamba pamoja na ratiba zetu zenye shughuli nyingi, tutahakikisha kwamba watoto wetu wanasoma kwa dakika 30 kila siku.
Ikiwa wazazi wenyewe hawawezi kusoma na watoto wao kwa sababu fulani, jaribu, tafadhali, kutoa miundo inayohitajika kwa haya kutokea. Unaweza kuomba msaada kwa walimu wa watoto wako, au uulize ndugu zake wakubwa kwake au watu wengine wa jamii. Hata watoto wadogo kabisa, ambao bado hawajaweza bado kusoma, wanapaswa kutumia wakati kuwa na vitabu kila siku – ama kusomewa, au kuwapa vitabu vya ma picha ili waangalie. Kwa njia hii, wataunda tabia ya kusoma na kujifunza utamaduni wa vitabu.