By Jean Damascene
Daktari Hawa Abdi, anayejulikana kwa wampendao kama Mama Hawa, alikuwa mtalaam wa mambo ya uzazi aliye sifiwa kuyaokoa maisha ya makumi elfu ya watu kwa mda wa miaka mingi. Kazi iliongezeka 30 thelathini sawa muda wa vita ya wenyewe kwa wenyewe vilivyo angamiza nchi. Daktari Abdi alifariki tarehe Agosti 5, 2020, hapa Mogadishu, akiwa na umri wa miaka 73, na kifo chake kime kumbukwa sana tena sana. Baada ya kusoma elimu ya utabibu kwa katika umoja wa Kisovieti, Dktari Abdi alikuwa mmoja wa wanawake wa kwanza wa kisomali kufanya hivyo. Alihitimu pia digrii ya sheria Kutoka Chuo kikuu cha Kitaifa cha Somali. Baadaye alianzisha Kliniki ndogo katika kijiji chake. Wakati vita vya wenyewe kwa wenyewe vilipoibuka mnamo mwaka wa 1990 na kutishia kugabula nchi, Daktari Hawa alibaki ndani ya Somali na polepole akaenda anabadilisha kliniki yake kuwa hospitali ya vitanda 400 iliyo watibu watoto, wanawake na wanaume. Alisaidia kila aliye kuwa ameafiriwa na vita kwenda kwa wamama waliojifungua uzazi. Alijenga pia shule la wanawake na shule la kilimo.
Katika nchi iliyo vamiwa na mgawanyiko wa kikabila, Daktari Abdi anasemekana kuweka kiwango: alitunza kila mtu kwa usawa, bila kuangalia kabila lake. Aliteuliwa tunzo la Amani la Nobel mnamo mwaka wa 2012, pia alipokea tunzo nyingine nyingi katika maisha yake, ikiwemo digrii ya Daktari wa sheria kutoka Chuo kikuu cha Harvard. Watoto wake wawili ambao sasa ni ma daktari, mmoja anaongoza hospitali aliyoiunda Dktari Abdi. Rais Mohamed Abdulahi Mohamed wa Somalia alizungumzia juu ya Daktari Abdi kwa chapisho lake la facebook, kama alikuwa “mutu aliye na nafasi nzuri kama ya dhahabu katika historia ya Somalia …Atakumbukwa kwa kazi alizozifanya wakati wa shida. Jarida la “Glamour” lilimueleza Daktari Abdi na binti yake daktari pia katika toleo la 2010 kama watakatifu wa Somalia, ikiwalinganisha na Mama Theresa
Mzaliwa wa kiSomali aishie Maine, Deqa Dhalac, ambaye sasa ni raia wa Marekani, amesema kwamba amefurahishwa na kazi Daktari Hawa Abdi ameifanyia Somalia. Kwa ujasiri wake wa ku kabiliana na vita, na kubaki nchini-akihatarisha maisha yake ili kuwasaidia maelfu ya wasiojiweza-ni ya beyi ghali sana. Walio wengi kati yetu wanadaiwa kumushukuru kwa mabadiliko aliyo fanya kwa watu wengi, amesema Dalaq, na kuongeza kuwa mtazamo wa Daktari Abdi umemchochea pia kujitahidi kuwa sauti kwa wasio na sauti.
The New York Time ili ripoti kwamba mwakani 2010 hospitali yake ime chukuliwa na wanamgambo wa kiislam. Baada ya kupora mahali hapo, wamepima kumushurutisha aondoke na kuacha kituo hicho cha afya, lakini alikataa na akashikilia ardhi yake. Kwa barua ya Facebook ya jumba la makumbusho la Somalia la Minesota inasomeka: “Daktari Abdi ni shujaa kwa mamilioni ulimwenguni, na urithi wake hautasahaulika”